GERVINHO AKAMILISHA ROMA

Mchezaji raia wa Ivory Coast Gervinho amekamilisha usajili wake kutoka Arsenal kwenda AS Roma ya Italia.Gervinho amesajiliwa na AS Roma kwa ada ya uhamisho inayokadiriwa kuwa Paundi Milioni 8. Gervinho alisajiliwa na Arsenal kwa paundi milioni 12 mwaka 2011 kutoka Lille ya Ufaransa. Mchezaji huyo amejiunga na Roma inayofundishwa na kocha wake wa zamani kipindi yuko Lille Rudi Garcia.
Designed by OddThemes | Distributed by Gooyaabi Templates