Paris Saint-Germain iko katika harakati za mwisho kupata saini ya mchezaji wa kimataifa wa Brazil anayekipiga Chelsea ya Uingereza David Luiz.
Kukamilika kwa uhamisho hu kutamfanya David Luiz kuwa beki ghali zaidi ulimwenguni huku Chelsea ikipata zaidi ya mara mbili ya kiasi walichotumia kumnunua kutoka Benfica. Chelsea na Benfica zilifikia makubaliano ya Luiz kwa kiasi cha Euro milioni 21.3 January 2011.
Uhamisho wa beki mwingine wa Kibrazil Thiago Silva kwenda PSG ndio unaoshikilia rekodi ya dunia kwa sasa na usajili wa Luiz utawafanya mabeki hao wawili wanaokipiga kwenye kikosi cha kwanza cha timu ya Brazil kuwa pamoja.
Luiz ambaye anajiandaa kushiriki kombe la dunia na timu yake ya taifa anatarajiwa kukamilisha usajili huo unaokadiriwa kuwa na thamani ya Euro milioni 50. Mchezaji huyo mwenye miaka 27 ameandika shukran zake kwa Chelsea katika ukurasa wake wa twitter huku ukurasa wa Chelsea ukithibitisha makubaliano kati ya PSG na klabu hiyo ya London.
Tks CFC for this time of great partnership. I'm thankful for all! It's a new challenge and together we ll go even further. Allez Paris!
— David Luiz (@DavidLuiz_4) May 24, 2014
We've agreed terms with PSG for the transfer of @DavidLuiz_4, subject to him agreeing terms & passing medical. http://t.co/r348ksJHRN #CFC
— Chelsea FC (@chelseafc) May 23, 2014


