APPLE YAPATA FAIDA ZAIDI YA $ BILIONI 13

Kampuni ya Apple yenye makao makuu yake Cupertino, California imetangaza faida ya zaidi ya dola bilioni 13 kutokana na mauzo ya bidhaa zake mbalimbali. Apple, wameuza zaidi ya simu milioni 51 aina ya Iphone pamoja na Ipad zaidi ya milioni 26 kwa robo ya mwaka.
Mkurugenzi wa Apple Inc. Tim Cook ameeleza kupanda kwa mauzo ya bidhaa za Apple huku mauzo hayo yakipanda kwa asilimia Amerika
Kusini kwa 76%, Afrika 65%, Japan 40%, Ulaya 115% na China mauzo yakipanda kwa 20%. Wachambuzi wa masuala ya biashara wanadai kuwa kwa Marekani pekee mauzo ya Apple yanazidi kushuka. Bidhaa ya mwisho kutengenezwa na Apple, Iphone 5 inafanya vizuri sokoni japo inakumbwa na ushindani mkubwa kutoka kwa Samsung S4 na simu ghali kuliko zote kati ya Iphone hizo ni Iphone 5s inayouzwa kwa $860 ambazo ni zaidi ya shilingi 1,300,000/=
Designed by OddThemes | Distributed by Gooyaabi Templates